Jumanne , 4th Apr , 2023

Watu saba wamefikishwa katika mahakama ya wilaya Manyoni na kusomewa shtaka la mauaji ya mtu mmoja ambaye hakufahamika anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 40 - 45 usiku wa machi  03.2023 wilayani Manyoni

Akisoma kesi hiyo namba 11 ya mwaka 2023 akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu mkazi mwandamizi Felician Kapama, mwendesha mashtaka upande wa Jamhuri mkaguzi msaidizi wa polisi  Ryoba Mkambala amesema kuwa kwa pamoja washtakiwa hao walishiriki kumuua mtu huyo

Washtakiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo
Hakimu Felician ameiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 18 April kesi hiyo itakapotajwa tena, huku washtakiwa wakirudishwa rumande kwakuwa kesi hiyo haina dhamana.