Alhamisi , 6th Oct , 2022

Waziri wa barabara nchini Sudan Kusini Bw. Simon Mijok Mijak ameomba radhi kwa wananchi wan chi hiyo kutokana na ubovu mkubwa wa barabara nchini humo ambao unatajwa kwamba ni wa aina yake.  

Barabara Sudan Kusini zimekua mbovu sababu ya mvua kubwa zinazoendela kunyesha ambazo zimesababisha njia kutopitika sababu ya mafuriko na matope.

Zaidi ya malori 1,500 yaliyobeba vyakula na  mahitaji ya msingi  yamekwama huko Magharibi mwa nchi hiyo.  

Waziri huyo amesema kwamba wakandarasi wanafanyia kazi suala hilo ikiwemo kuharakisha malori kufika eneo la wahitaji

Barabara za Sudan Kusini zinatajwa kwamba ni mbovu kwenye ukanda wa Afrika  kwa mujibu wa ripoti i liyotolewa na Bodi ya mamlaka ya usafiri Mashariki na Kaskazini  mwa Afrika (NCTTCA).