
Jeneza la Marehemu Adam Kuambiana katika viwanja vya Leaders Club wakati wa shughuli ya kumtolea heshima za mwisho.
Maziko ya msanii huyu yameongozwa na viongozi mbalimbali akiwepo Waziri Wa Habari Vinana Tamaduni na Michezo Dr Fenella Mukangara, Mstahiki Meya wa Wilaya ya Kinondoni
Maziko ya masanii huyu ambaye umaarufu wake mkubwa umetokana na ushiriki katika filamu kama vile Fake Pastors, Fake Sons, na Regina, yametanguliwa na shughuli ya utoaji heshima za mwisho kwa mwili marehemu iliyofanyika katika viwanja vya Leaders Club Jijini Dar es Salaam.
Wakitoa maneno yao ya mwisho kwa Marehemu na kwa waliohudhuria msiba huu, kwa niaba ya wengine Mheshimiwa Waziri amewataka wasanii kuendeleza moyo wa Marehemu Adam katika kuendeleza wasanii kimasomo.
Marehemu ameelezwa kupoteza maisha kutokana na tatizo la Vidonda vya Tumbo.
Vilevile JB, Jokate, Mtunis kati ya wengine hapa wanaeleza namna Adam alivyokuwa mtu wa kipekee kwao, wakimpa sifa ya Muongoza filamu namba moja Tanzania.