Alhamisi , 3rd Jun , 2021

Klabu ya soka ya Inter Milan imemtangaza rasmi Simone Inzaghi kuwa kocha wake kwa kipindi cha miaka miwili kutoka sasa.

Simone Inzaghi kocha mpya wa Inter Milan

Inzaghi amejiunga na timu hiyo akitokea timu ya Lazio, anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Antonio Conte aliyeondoka klabuni hapo wiki moja iliyopita baada ya kuwapa ubingwa wa msimu wa 2019/2020.

Inzaghi ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa vilabu vya  Lazio , Sampodoria Atalanta na timu ya Taifa ya  Italia iliitengeneza timu hii na kuifanya kuwa shindani katika msimu huu wa serie A

Mafanikio yake akiwa na  Lazio msimu huu, ni kumaliza katika nafasi ya 6 msimamo wa serie A  akiwa ameshinda michezo 21 kati ya 38  imesare 5 na kupoteza 12 imemaliza ikiwa na alama 68 .