Mchezo wa Simba na Yanga
Malinzi pamoja na aliyekuwa Katibu wa shirikisho hilo, Selestine Mwesigwa walikuwa akikabiliwa na mashtaka kadhaa likiwemo la utakatishaji fedha, kabla ya kufikia mwisho mwezi Disemba 2019 kwa kupokea hukumu ya jela miaka miwili au kulipa faini ya shilingi laki 5 baada ya kukutwa na hatia, ambapo wamekubali kulipa faini.
Malinzi ameibuka hii leo katika ukurasa wake wa Twitter, ikiwa ni siku kadhaa baada ya kumalizika kwa mchezo wa Simba na Yanga, ambapo amewashukuru wadau wa soka na mitandao mbalimbali barani Afrika kwa kuutangaza mchezo huo.
Pia ametoa ushauri kuwa jambo hilo linahitajika kufanyika mara kwa mara ili kukuza ubora wa mchezo huo pamoja na mapato.
Dear friends on the continent,thank you for promoting this match and indeed our local league.More of it is needed so as to improve the level of the game and its financial position. https://t.co/mki8gDVGdG
— Jamal Malinzi (@jamalmalinzi) January 7, 2020
Mchezo huo wa Simba na Yanga unakadiriwa kuingiza takribani watazamaji 58,000 ikiwa ni mahudhurio makubwa zaidi ya watazamaji katika mechi ya vilabu Afrika Mashariki.