Ijumaa , 27th Feb , 2026

Mshambuliaji wa Simba, Jonathan Sowah, amezungumza baada ya kuibuka taarifa za kuondolewa kambini na klabu na kuamuriwa kurejea Dar es Saalam watakti timu ilipokuwa Dodoma.

Jonathan Sowah

Sowah amesema hajawahi kukosa nidhamu na hajui sababu za madai yanayomzunguka kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii hivi karibuni

Sowah aliongeza kuwa alijipanga kuendelea kuitumikia Simba baada ya kumalizika adhabu yake ya mechi tano, lakini alishangazwa na taarifa za kumrudisha Dar es Salaam.

“Sijajua kwanini nimeambiwa nirudi Dar, nimesubiri kikao cha uongozi kujua ukweli,” - Sowah

Sowah aliingia Simba msimu huu akitokea Singida Black Stars, akitokea na rekodi nzuri ya mabao 13 katika mechi 14, akitarajiwa kuongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji ya Simba.