
Bingwa huyo mtetezi wa Australian, alikuwa na alianza taratibu aliporejea uwanjani kwa mara ya kwanza baada ya miezi minne lakini bado alifuzu kwa raundi ya pili ya mashindano ya Melbourne Summer Set kwa ushindi wa 6-4 3-6 6-3 dhidi ya Alize Cornet asubuhi ya leo Jumanne.
Osaka, ambaye mara ya mwisho alicheza kwe michezo ya ushindani alipofungwa na Leylah Fernandez katika raundi ya tatu ya U.S. Open Septemba mwaka jana, alionyesha kurejea kwa nguvu lakini mara nyingi alikosa usahihi katika michuano hiyo ya kujiandaa kwa Australian Open.
Mjapani huyo anatazamia kurejesha makali yake kwenye michuani ya wazi ya mwaka huu yatakapoanza siku ya Januari 17 mjini Melbourne.