
Nyota wa Tennis wa England Emma Raducanu
Raducanu mwenye umri wa miaka 19 ambaye anashikilia taji la ubingwa wa michuano ya wazi ya Marekani (US Open) amesema ni mapema sana kufikiria kuhusu mkufunzi wake mpya huku tangu anyakuwe ubingwa wa US Open amekuwa akiandamwa na majeraha yaliyosababisha kutolewa mapema kwenye michuano mbalimbali aliyoshiriki kwa mwaka 2022.
Nyota huyo anayekamata nafasi ya 11 kwa viwango vya ubora duniani amesema ndoto zake za siku za mbeleni kucheza pamoja na Muingereza mwenzake Andy Murray kama timu moja kama ambavyo Murray alicheza na Serena Williams mnamo mwaka 2019