
Kocha wa Simba Sven Vandenbroeck
Kupitia kurasa za mitandao ya kijamii, Simba wameweka takwimu za matokeo ya mechi mbili alizofundisha kocha wao mpya Sven Vandenbroeck.
Mechi 2⃣
Ushindi 2⃣
Magoli tuliyofunga 1⃣0⃣
Magoli tuliyofungwa 0⃣
Tunaendelea kuhesabu tarehe ya sisi na wao #NguvuMoja pic.twitter.com/LVs27SNRKz— Simba Sports Club (@SimbaSCTanzania) December 26, 2019
Katika mechi hizo mbili Simba imeshinda zote na kufunga jumla ya magoli 10 huku ikiwa haijaruhusu kufungwa goli.
Simba imeshinda goli 6-0 dhidi ya Arusha FC kwenye kombe la shirikisho na ikashinda 4-0 dhidi ya Lipuli FC kwenye mchezo wa ligi kuu siku ya jana Disemba 25, 2019.
Yanga na Tanzania Prison zitacheza kesho kwenye uwanja wa Samora Iringa. Mbali na hilo uwanja wa Sokoine umefungiwa na Bodi ya ligi kutumika katika mechi za ligi kuu, ligi darala la pili na ligi daraja la kwanza.