Ijumaa , 23rd Mei , 2014

Nyota wa miondoko ya muziki wa injili nchini Kenya Emmy Kosgei na Bahati Bag wamekuwa ni miongoni mwa wanamuziki mbalimbali waliotajwa kuwania tuzo za "Africa Muziq Magazine" (AFRIMMA).

Emmy Kosgei

Wawili hao wametajwa kuwania katika kipengele cha msanii bora wa muziki wa injili barani Afrika huku wakichuana na wasanii Nikki Laoye kutoka Nigeria, Ntokozo Mbambo Africa Kusini, Sonnie Badu wa Ghana na Icha Kavons kutoka Congo.

Sherehe za utoaji tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika tarehe 26 mwezi Juni mwaka huu jijini Dallas, Texas nchini Marekani.