
Waziri wa Habari, Nape Nnauye
Taarifa hiyo ameitoa hii leo Januari 31, 2022, na kusema kuwa mabadiliko yaliyofanyika ni ya kanuni namba 18 ya mwaka 2018, na kusema kuwa Rais Samia amemwagiza kufanya mabadiliko na kanuni zimeshasainiwa na tayari zimeanza kutumika ili kuongeza wigo kwa Watanzania kupata habari.
"Tumefanya mabadiliko, chaneli ambazo hazilipiwi zianze kuonekana kwenye king'amuzi cha DStv, mtakumbuka baadhi ya chaneli ziliondolewa kwenye king'amuzi chenu na hili jambo limekuwa kilio kikubwa kwa wananchi, Rais kaniagiza na nimefanya mabadili," amesema Waziri Nape