Jumatatu , 28th Nov , 2022

Jumla ya wagonjwa wa macho 40, wilayani Kiteto mkoani Manyara, watafanyiwa operesheni kufuatia kuwa na matatizo mbalimbali ya macho yakiwemo mtoto wa jicho, mtindio wa maji kwenye macho na vimbe mbalimbali.

Baadhi ya wananchi wanaotarajiwa kufanyiwa upasuaji

Operesheni hizo zinafanyika hii leo Novemba 28, 2022 kituo cha afya ADK Kiteto chini ya Kanisa la Anglicana Kiteto.

Huu ni mwendekezo wa huduma zinazotolewa na Kituo hicho ambapo jumla ya watu 776 walifanyiwa operesheni kubwa za macho na 405 walifanyiwa operesheni ndogo kati ya mwaka 2006 hadi 2022.

Akizungumza na wagongwa hao Askofu wa Kanisa la Anglicana Kiteto Isaya Chambala, amesema lengo la kanisa hilo pamoja na kuwasaidia waamini kiroho na kimwili ambapo pia huduma za Afya zinaendelea kutolewa