Jumanne , 9th Mei , 2023

Watalaamu kutoka Shirikisho la soka barani Afrika CAF wameendelea na ufungaji vifaa vya teknolojia Assistants Referee (VAR) kwa ajili ya mchezo wa robo fainali baina ya Yanga dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini utakaochezwa jumatano Mei 10,2023 majira ya saa 10 jioni

Yanga na Muramo kuamuliwa VAR.

Akitoa taarifa hiyo Kaimu meneja wa uwanja wa Mkapa , Milinde Mahona kuwa maandalizi yanakwenda vizuri na wataalamu hao hawajapata changamoto yoyote katika ufungaji wa vifaa hivyo kila kitu kinakwenda Vizuri.

'' Maandalizi yanakwenda vyema kwa kila mtu kuwajibika kwenye nafasi hivyo, mashabiki wajitokeze kutoa hamasa kwa timu yao '' Mahona Kaimu Meneja Uwanja Benjamin Mkapa

Pia kaimu  huyo ametoa rai kwa mashabiki kuwa wazalendo pindi wanapokwenda uwanjani hususani kutunza miundombinu ya uwanja huku hatua kali zaidi zitachukuliwa kwa wale wenye tabia ya kuvunja au kuharibu miundombinu ya uwanja.

Kwa upande mwingine  Afisa habari wa Yanga Ally Kamwe amesema  ni kweli wamepokea barua  kutoka Shirikisho la soka barani Afrika ya kwa kupigwa faini ya jumla ya Dola 35,000 na Caf ambayo ni zaidi ya Sh 82 milioni kwa makosa mbalimbali yanayodaiwa kufanywa katika mechi yao ya robo fainali kati yao na Rivers United ya Nigeria.

''Uongozi wa Yanga umekutana na leo umekata rufaa kupiga maamuzi hayo hivyo tunawasubiri nini ambayo watajibiwa na CAF ''amesema Kamwe Afisa habari Yanga