Mbeya City yaingia 5 bora, Ligi Kuu
Klabu ya Mbeya City imepanda kwenye msimamo wa Ligi kuu Tanzania bara kutoka nafasi ya 7 hadi ya 5 imefikisha alama 28. Wamepanda baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Biashara United kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya leo April 28.