Bayern, Liverpool kuwakosa nyota watatu UEFA
Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya itaendelea usiku wa leo kwa michezo miwili ya mkondo wa pili ya mtoano hatua ya 16 bora, ambapo kalabu ya Bayern Munchen itacheza na RB Salzburg baada ya sare ya 1-1 wakati Liverpool itacheza na Inter Milan ikiwa na faida ya Ushindi wa 2-0 ugenini.

