RC Mbeya aunda tume kuchunguza kifo cha dereva
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila ameunda tume ndogo ya watu wanne na kuipa jukumu la kuchunguza kifo cha dereva wa Lori aliyefahamika kwa jina la Abdulhman Issa anayedaiwa kufia mikononi mwa polisi katika eneo la Shamwengo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.