Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali kuiuzia Dangote gesi asilia kwa miaka 20

Monday , 20th Aug , 2018

Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini TPDC, kupitia Kaimu Mkurugenzi Mkuu wake Mhandisi Kapuulya Musomba, limesaini mkataba wa miaka 20 wa kukipatia kiwanda cha saruji cha Dangote, gesi asilia kama nishati kwa ajili ya kuzalisha saruji.

Kiwanda cha Dangote.

Kufuatia makubaliano hayo yaliyosainiwa jijini Dar es salaam hii leo, kiwanda cha Dangote kitaacha matumizi ya nishati ya mafuta katika uzalishaji na kwamba mchakato wa kuhama kutoka matumizi ya mafuta kwenda ya gesi utachukua kati ya siku 30 hadi siku 45 kuanzia sasa.

Hivi karibuni kumekuwa na uhaba wa saruji katika soko ambapo kwa mujibu wa Waziri wa Viwanda Mh. Charles Mwijage, moja ya sababu ni kupungua kwa uzalishaji wa kiwanda cha Dangote hivyo kusainiwa kwa makubaliano hayo kutasaidia kupunguza kuadimika kwa bidhaa ya saruji katika siku za usoni.

Mradi wa gesi asilia na iliyosindikwa Tanzania (TGP) ni miongoni mwa miradi mikubwa zaidi ya ujenzi wa miundombinu katika historia ya Tanzania matumizi ya gesi iliyopo nchini yataongeza uwezo wa nchi wa kusafirisha nje rasilimali hiyo na kuboresha miundombinu ya ndani.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton