Wednesday , 2nd Nov , 2016

Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal ameonya kuwa uvuvi haramu unaofanywa na wavuvi katika maeneo ya pwani ya bahari ya Hindi unatishia kutoweka kwa matumbawe jambo ambalo lina madhara makubwa ya mazingira ya nchi.

Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Gharib Bilal

 

Akiongea katika kongamano la mazingira na mabadiliko ya tabia nchi lililoandaliwa na Kigoda cha Mwalimu cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amesema kitendo cha kuendelea kufanya hivyo kunaharibu matumbawe ambayo yana umuhimu katika fukwe na viumbe wengine wa baharini.

Dkt. Bilal amesema kama hatua za haraka hazitachukuliwa kudhibiti uvuvi haramu wa kutumia baruti, Janga kubwa la kimazingira litatokea na hivyo kuathiri shughuli za kiuchumi na ustawi wa jamii.

Dkt. Bilal ameongeza kuwa uvivu haramu unakimbiza samaki lakini pia unaathiri maisha ya watu ambao uchumi wao unategemea rasimali za baharini.