Tuesday , 3rd May , 2016

Wafanyabiashara wanaotumia Bandari ya Dar es salaam kwa shughuli ya kusafirisha na kuingiza mizigo wame shauriwa kuhakikisha kuwa wanaandaa Nyaraka na kufuata taratibu za ushuru ili kuondokana na usumbufu wa kukwama kwa mizigo bandarini hapo.

Akiongea na East Africa Radio katika mahojiano maalumu jijini Dar es salaam,Rais wa chama cha mawakala wa forodha nchini TAFA Bwana Steven Ngatunga amesema, wafanyabiashara wengi hupata hasara na kuingia garama zisizo zalazima kutokana na kutokuwa na nyarama muhimu.

Bwana Ngatunga amesema, ili kuepuka usumbufu hasa kwa wafanyabiashara kutoka nje ya nchi ni vyema kuonana na wakala wa forodha aliyesajiliwa kuweza kupata msaada wiki mbili kabla ya meli yamizigo kuwasili bandarini hapo.