Tuesday , 1st Nov , 2016

Jumla ya watahiniwa 408,442 wameanza leo kufanya mtihani wa kidato cha nne 2016 katika shule za sekondari 4,727 ambazo zinatarajiwa kuanza kufanya mtihani huo tarehe 01 hadi 18 Novemba 2016.

Wanafunzi wakiwa katika chumba cha mtihani

Akitoa taarifa ya kuanza kwa mtihani huo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani Tanzania, Dkt. Charles Msonde, amesema maandalizi yote ya kufanyika kwa mtihani huo yamekamilika huku akitoa onyo kwa watakaojaribu kufanya udanganyifu katika mitihani hiyo.

Dkt. Msonde amesema matokeo ya mtihani huo yatatumika katika uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na elimu ya juu ya kidato cha tano, kupata wataaluma wa fani mbalimbali kama vile afya, kilimo, ualimu na ufundi.