Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waliomshambulia Lissu wasamehewa

Monday , 20th Nov , 2017

Mke wa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, Alicia Magabe amesema amewasamehe watu waliofanya shambulio la kumpiga risasi Mume wake ingawa bado anataka haki itendeke ikiwa ni pamoja na kufahamu walifanya kwa lengo gani na nani amewaagiza.

Bi. Magabe ameyazungumza akiwa Nairobi kwenye mahojiano maalumu na gazeti la hapa nchini ambapo amesema kwamba “Binafsi nimewasamehe kwa kitu walichokifanya, lakini hiyo haina maana kwamba nisingependa kuona haki inatendeka,” alisema wakili huyo.

Ameongeza “Sitaki kuwe na mkanganyiko baina ya kusamehe na hali ya kutamani kuona haki inatendeka. Tukio hilo limemfanya nianze kuamini kuwa kuna watu walitaka kumuua Lissu, lakini hawajafanikiwa na naaamini watu hao wapo, hivyo nahofia usalama wa familia yangu".

Hata hivyo mwanamama huyo amesema kwamba mpaka sasa hajasikia kama uchunguzi wowote umefanyika au waliohussika na tukio wamekamatwa hali inayopmfanya yeye kuwazia usalama wa mumewe pamoja na yeye kama mke kwani hafahamu watu hao kwa sasa wanawaza nini.

Lissu akiwa na Mke wake Hospitali (Nairobi alipolazwa)

Akizungumzia hali ya mume wake tangu alipopata matatizo Bi Magabe amesema kwamba baada ya Lisu kupata fahamu sawasawa ari yake ipo juu sana na wala hana unyonge wala uwoga juu ya yale yaliyomtokea huko nyuma.

"Si mtu wa kusema kuwa baada ya tukio amekuwa mnyonge, mwoga au ujasiri wake umepungua. Sijawahi kupata hata kauli yake moja inayoashiria kwamba sasa atarudi nyuma. Kama mke nataka mume wangu apone, tutoke hospitali turudi nyumbani. Lakini wanapokuja viongozi wenzake kutoka Tanzania, wastaafu na wa sasa na hata hapa Kenya, kauli zake zote zinaashiria amekua zaidi kisiasa." Wakili Magabe.

Ameongeza “Anasema ‘kuna siku nitapona na nitaendelea na kazi zangu’ ili kuwatia moyo wanasiasa na wanaharakati".

Lissu alipigwa risasi Septemba 07 mwaka huu akiwa mkoani Dodoma maeneo ya nyumbani kwake Area D na watu wasijulikana na baadaye alipelekwa Jijini Nairobi, Kenya kwa ajili ya matibabu zaidi.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita