Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tundu Lissu aikataa nafasi ya U-makamu wa rais

Thursday , 14th Mar , 2019

Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Antiphas Lissu amesema hana mpango wa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi, hivyo anastahili kuendelea kupatiwa stahiki zake za ubunge zikiwepo posho na mshahara.

Mbunge Tundu Lissu

Lissu amesema hana mpango wa kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi, hivyo anastahili kuendelea kupatiwa stahiki zake za ubunge zikiwepo posho na mshahara.

Lissu aemeyasema hayo wakati akielezea vifungu vya sheria vilivyopo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba katika Ibara ya 71, moja ya jambo ambalo litamfanya Mbunge kukoma kupatiwa stahiki zake ni pale anapoteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa nchi.

Jana Februari 13,  Lissu amethibitisha kuwa uongozi wa Bunge kupitia kwa spika, Job Ndugai na katibu wake Steven Kagaigai umemfutia rasmi mshahara na posho za kibunge kwa kile alichoeleza kuwa ofisi ya spika haina taarifa za anachokifanya nje ya nchi.

"Katika Katiba ya nchi, Ibara ya 71 kati ya sababu zilizotajwa na ibara hiyo, sababu ya sita inasema endapo ukiteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa rais, hutapata stahiki za kibunge. Mimi sitajii kuteuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais", amesema.

Pamoja na sababu mbalimbali alizozitaja Mbunge huyo zitakazopelekea kunyimwa stahiki zake za Kibunge amesema hakuna sababu yoyote inayomfunga hivyo Bunge linapaswa kumpatia stahiki zake kwani kama ni kutokuwepo kwake bungeni, Spika Ndugai alikuwepo katika kikao kilichoadhimia yeye apelekwe Nairobi kwa matibabu wakati alipokuwa hoi baada ya kupigwa risasi Septemba 07, 2017.

Mbali na hayo Lissu amesema ameshawasiliana na wanasheria wake walipo Tanzania waweze kufungu mashtaka dhidi ya Bunge kwa kuzuia mishahara na posho zake.

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ