Yahia Kallash, kiongozi wa chama cha waandishi wa habari nchini Misri
Hukumu hiyo, ambayo inaweza kufutwa wakilipa faini ya dola mia sita, imetokana na msako wa polisi kwenye ofisi ya jumuiya ya wafanyakazi mjini Cairo mwezi wa Mei, wakati polisi wa nchi hiyo walipokuwa wakiwasaka waandishi wa habari wawili.
Wanahabari waliokamatwa walishutumiwa kulalamika juu ya uamuzi wa serikali ya Misri, kuikabidhi Saudi Arabia, visiwa viwili katika Bahari ya Sham.

