Wednesday , 4th May , 2016

Wasanii wa Double M Plus wameamua kumwagana damu na kuikimbia bendi yao baada ya uongozi huo kukalia mishahara yao.

Wasanii wa Double M Plus Salehe Kupaza na Dogo Rama

Wakizungumza na Enewz kwa nyakati tofauti wasanii hao walieleza kuwa mkasa mzima ulitokana na kiongozi wa bendi hiyo Mumini Mwinjuma kuacha kuwalipa kwa muda mrefu na kuwapatia posho tu.

“Ni kawaida yake Mumuni kuwadhurumu wasanii kwasababu hata wasanii wake wa mara ya kwanza Double M Sound ilikuwa hivyo hivyo walikuwa wanaishi kwa posho mwisho wa siku mishahara hawakupatiwa”, alisema Salehe Kupaza

Akielezea sababu iliyomfanya amtwange mangumi bosi wake 'Muumi', Kupaza alisema kuwa ni hasira alipokuja kugundua kuwa hata wao watakuwa wametapeliwa kama alivyokuwa amefanya kwa wa mara ya kwanza 'Double M Sound'