Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Maneno ya kwanza ya muigizaji Lulu

Friday , 16th Nov , 2018

Msanii wa filamu nchini aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia, Elizabeth Michael (Lulu) amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kuachiwa huru Novemba 12.

Msanii Elizabeth Michael (Lulu).

Kupitia ukurasa wake wa 'Instagram' Lulu ametoa shukurani kwa kila aliyeshiriki kumuombea na kumshika mkono kwa namna yoyote ile katika kipindi chake chote cha kesi yake.

Lulu ameandika, "Kwa dhati kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru kila aliyeshiriki kuniombea katika kipindi kigumu sana kwangu, kwa familia yangu na watu wangu wa karibu, mliolia na kusali pamoja na mimi ni wengi mno, ninaowajua na nisiowajua".

Ameongeza kuwa, "Kilikuwa kipindi chenye maumivu, matusi, dharau, hukumu za wanadamu, maneno ya kulaaniwa, majina yasiyofaa na mambo mengi ya aina hiyo, lakini nashukuru Mungu sikuyapokea kama yalivyo bali niliyapokea kama shule au somo lililojaa utukufu wake".

Lulu ameendelea kwa kusema kuwa kile kilikuwa ni kikombe na ilikuwa ni lazima akinywe, yalikuwa majira ambayo ni lazima ilikuwa apitie na mwisho yakawa mapenzi ya Mungu na yametimizwa.

Lulu alikuwa akitumikia kifungo cha miaka miwili jela, baada ya Novemba 13, mwaka jana kuhukumiwa na mahakama kuu baada ya kupatikana na hatia ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa gwiji wa filamu, Steven Kanumba.

Hata hivyo, Aprili 26 mwaka huu, msanii huyo alibadilishiwa adhabu hiyo na kuwa ya kifungo cha nje. Kutokana na hilo, alipangiwa kazi ya kufanya usafi katika Wizara ya Mambo ya Ndani iliyopo maeneo ya Posta Jijini Dar es salaam aliyoianza tangu Mei 14 mwaka huu. 
 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita