
Adi Yussuf (katikati) akiwa na mabosi wa Blackpool
Adi ambaye amewahi kuitwa timu ya taifa ya Tanzania, amekuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na timu hiyo katika majira haya ya kiangazi.
Nyota huyo mwenye umri wa 27, anajiunga na timu hiyo inayoshiriki League One nchini England, akitokea Solihull Moors ambayo inayoshiriki National League ya nchini humo.
Amefunga magoli 21 katika michuano yote msimu huu akiwa na Solihull, magoli mawili kati ya hayo ameyafunga kwenye mechi dhidi ya Blackpool katika michuano ya FA Cup.
@adiyussuf | "This is a dream come true for me. All the hard work and sacrifices I've made this year have paid off." pic.twitter.com/pZzSuLFs2Q
— Blackpool FC (@BlackpoolFC) May 28, 2019