
Kwenye ukurasa wake wa twitter Museveni ameandika ujumbe huo wa kuwatakia kila la heri The Cranes, akisema kwamba licha ya kwamba timu hiyo imeshafuzu kucheza fainali za AFCON, lakini wahakikishe kuwa hawapotezi mechi yao dhidi ya Tanzania.
Kauli ya Museveni ilimfanya Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zuberi Kabwe kuibuka, na kumtaka Museveni kuacha roho mbaya na kutoibania Tanzania, huku akimkumbusha kuwa mafuta yao yanapita nchini Tanzania.
Even if the Cranes have already qualified, I know that they still have a game to play against Tanzania. Please make sure you do not lose that game. Congratulations once again. pic.twitter.com/e3G1ATkNDz
— Yoweri K Museveni (@KagutaMuseveni) November 20, 2018
Mzee acha roho mbaya. Mmeshasahau mafuta yenu yanapita Tanzania? Shauri yako
— Zitto Kabwe Ruyagwa (@zittokabwe) November 20, 2018
Timu ya Taifa ya Tanzania inatarajia kucheza na The Cranes ya Uganda mwezi Machi, 2019, ambapo iwapo itashinda itakuwa wamepata tiketi ya kushiriki michuano ya AFCON, ambayo inatarajia kufanyika mwaka 2019 nchini Camerron.