Mchezo uliochezwa muda mfupi uliopita Taifa Stars walianza kuongoza kwa kupata goli kupitia Erasto Nyoni ndani ya dakika 15 za mwanzo wa mchezo na baadaye kuja kusawazishwa na Brian Mwila dakika ya 43.
Hata hivyo hali kwa upande wa Taifa Stars ilizidi kuwa mbaya baada ya kukubali Justin Shonga kutingisha nyavu dakika ya 45 na kuendeleza mashuti ambapo kati ya magoli matatu aliyoyafunga moja liilikuwa la mkwaju wa penati.
Magoli ya Tanzania yamefungwa na Erasto Nyoni dakika 15 pamoja Saimon Msuva dakika ya 84
Taifa stars wanatarajiwa kucheza mechi ya kuwania nafasi ya mshindi wa tatu na timu itakayofungwa kwenye mchezo kati ya Zimbabwe na Lesotho ambao watacheza leo huko huko Afrika Kusini.



