Wachezaji wa Taifa Stars kushoto na Zitto Kabwe kulia
Zitto kupitia mtandao wa Twitter ameweka ujumbe huo, akitamani wachezaji hao wasingepata taarifa za kutekwa kwa mfanyabiashara huyo ambaye pia ni mdau wa michezo nchini akiwa mlezi wa Simba SC.
Mo Dewji ambaye ni mwekezaji katika klabu ya soka ya Simba akimiliki asilimia 49 ya hisa za klabu ametekwa Alhamis Oktoba 11, 2018. Hadi sasa hajapatikana.
Taifa Stars jana usiku ulifungwa mabao 3-0 na wenyeji wao Cape Verde kwenye mchezo wa tatu wa kundi L, kuwania kufuzu fainali za AFCON 2019 zitakazo fanyika nchini Cameroon.
Tanzania sasa inashika nafasi ya mwisho kwenye kundi L ikiwa na alama 2 sawa na Lesotho inayoshika nafasi ya tatu ikiwa na alama 2 lakini ina wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa. Uganda wapo kileleni wakifuatiwa na Cape Verde zote zikiwa na alama 4.