Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Zahera anavyowapoteza mashabiki wa Yanga

Wednesday , 15th May , 2019

Licha ya ushindi mwembamba wa jana dhidi ya Ruvu Shooting, kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera ameedelea kubebesha mzigo wa lawama kwa waamuzi na Bodi ya Ligi.

Kocha Mwinyi Zahera (katikati) akisalimiana na Mwenyekiti mpya wa Yanga, Dk Mbette Msolla.

Mara kadhaa, Zahera amekaririwa akiwalaumu waamuzi pamoja na uongozi wa Bodi ya Ligi kuwa wanaikandamiza klabu hiyo katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Baada ya kumalizika kwa mchezo huo dhidi ya Ruvu Shooting, na Yanga kuibuka na ushindi mbembamba wa bao 1-0 kupitia kwa Papy Tshishimbi, kocha Zahera amesema, "malalamiko yangu yapo katika pande mbili, kwanza ni kwa upande wa marefa, wapo wanaokuja wakisema kuwa leo Yanga hatoki".

"Namna nyingine ni kwamba kuna mpango katika timu za Simba na Yanga. Sisi tunacheza FA tarehe 6, Azam FC anacheza na sisi tarehe 29, Lipuli na KMC nao wanacheza FA, lakini hakuna mtu ambaye anacheza ligi wakati anatakiwa kucheza nusu fainali ya FA ni Yanga peke yake", ameongeza.

Tuhuma za Zahera za klabu yake kuonewa limekuwa likibebwa kwa nguvu hadi na mashabiki wa klabu hiyo, wakiamini kuwa ubingwa wa msimu huu wataukosa kutokana na figisu za waamuzi na Bodi ya Ligi ambayo wanaituhumu kuipendelea klabu ya Simba.

Mwinyi Zahera amekuwa akionekana kuwa muwazi hadi kupitiliza na wadau wengi wa soka wanakosoa kitendo hicho kwa kuwa kinamharibia taaluma yake kama mwalimu. Wengi wanaamini majukumu yake ni kuzungumzia mafanikio na mapungufu ya kiufundi ya timu yake pamoja na wachezaji wake, badala ya kujihusisha na malalamiko ambayo yanatakiwa kuwasilishwa kwa Bodi ya Ligi kupitia njia sahihi na uongozi wa klabu.

Yanga hivi sasa inaongoza ligi ikiwa na alama 83 baada ya kucheza jumla ya michezo 36, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 82 ambayo imecheza michezo 33.

Bonyeza hapa chini kumsikiliza kocha Zahera.
 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ