Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya ubingwa, Kocha Mchenga amzuia Baraka

Friday , 11th Oct , 2019

Kocha wa Mchenga Bball Kings ambao ni mabingwa wa michuano ya Sprite Bball Kings 2019, Mohamed Yussuf 'Mudi' amesema kuwa wapinzani wasitarajie kuwa staa wa timu hiyo Baraka Sadick anaweza kuondoka.

Kocha wa Mchenga (wa kwanza kushoto), MVP Baraka Sadick (wa tatu kutoka kulia) wakiwa na baadhi ya mashabiki

Ameyasema hayo katika kipindi cha Dadaz kinachoruka kupitia EATV, ambapo amesema kuwa anamfahamu vizuri Baraka Sadick tangu akiwa kijana mdogo kipindi alipokuwa akija katika mazoezi yake.

"Awali kabisa wakati mimi nacheza kikapu, wao (Baraka na wenzake) walikuwa wanakuja wakiwa wadogo wananiona nacheza, tukishamaliza na wao wanaingia uwanjani wanarusha mipira. Nimekuwa mfano bora kwake, simaanishi nimehusika asilimia 100 lakini nimemfundisha", amesema Mudi.

"Kina Baraka hawawezi kuondoka Mchenga kwa sababu mimi nipo, hiyo ipo hata kwa Tamaduni kuna watu wa aina hiyo, mfano yule Stefano wa Tamaduni niliwahi kumfuata akaniambia subiri baada ya wiki na hatimaye siku zikapita nyingi mwisho akaniambia siwezi kuacha hapa na mimi nikamuelewa", ameongeza.

Akizungumzia ushindani aliokutana nao dhidi ya Taamaduni na fainali ngumu kwake, Mudi amesema, "katika game za fainali mwaka huu dhidi ya Tamaduni, game ya kwanza ndiyo ilikuwa hatari zaidi kwetu, walikuwa na nafasi ya kushinda. Tulikuwa tukiwazidi wanarudisha ilikuwa ngumu sana".

Mchenga wameshinda ubingwa baada ya kushinda michezo mitatu ya fainali dhidi ya Tamaduni, na kujishindia kitita cha Sh. milioni 10 na Tamaduni wakijishindia Sh. milioni 3. Mchezaji Baraka Sadick ameshinda tuzo ya MVP kwa msimu wa pili mfululizo na kujishindia Sh. milioni 2.

 

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa