Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baada ya milioni 500, Mo Dewji atoa tena 100

Tuesday , 10th Dec , 2019

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba Mohammed Dewji, ameahidi kutoa shilingi Milioni 100, kama zawadi kwa timu ya taifa ya Tanzania Bara Kilimanjaro Stars endapo itatwaa ubingwa wa CECAFA.

Mohammed Dewji

Mo Dewji ameyasema hayo jana usiku, alipotembelea kambi ya timu hiyo nchini Uganda, ambako michuano hiyo inafanyika, na kuwataka wachezaji wajitume zaidi ili waweze kupata ubingwa huo.

'Kama Mtanzania ambaye napenda kuona nchi yangu inafanya vizuri kwenye mchezo wa soka nimeahidi kutoa zawadi ya Tsh. 100m na zawadi ya pikipiki za Boxer kwa wachezaji na benchi la ufundi la timu yetu ya Tanzania Bara iwapo itashinda ubingwa wa michuano ya Cecafa ambayo inafanyika hapa nchini Uganda', alisema Mo Dewji.

Hatua hiyo ya kuahidi kiasi hicho cha pesa, imekuja siku moja baada ya kuahidi kutoa Milioni 500 kwenye awamu ya pili ya ujenzi wa uwanja wa Bunju Complex ambao umepewa jina la MO Simba Arena.

Ahadi hiyo alitoa siku ya Jumapili Desemba 8, 2019 kwenye mkutano mkuu wa Simba uliofanyika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam.

Kilimanjaro Stars leo inacheza na Zanzibar Heroes ukiwa ni mchezo wa pili baada ya ule wa kwanza kufungwa 1-0 na Kenya.
 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto 

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa