Baadhi ya washindi wa Television katika droo ya pili ya shindano la shinda na maji ya Kilimanjaro kutoka kampuni ya Bonite Bottlers zilizotolewa siku ya Leo Mikocheni jijini Dar Es Salaam.
Zawadi hizo zimetolewa kwa washindi hao kupitia droo ya pili ya shindano hilo, ambalo limedumu kwa muda wa wiki nane lililohusisha mikoa ya Dar Es Salaam, Pwani na Morogoro.
Akizungumza na EATV & EA Radio Digital, Msimamizi wa Mauzo na Masoko kutoka Bonite Bottlers Joseph Semali ameeleza kuwa,
Pikipiki ambazo wamekabidhiwa washindi
"Leo hii tumefanya hitimisho la droo yetu ambayo imedumu kwa wiki 8 ambayo ilianza Oktoba 7, hadi Novemba 30, 2019, ambapo tulipata jumla ya washindi 90, kati ya hao 45 tulishawakabidhi zawadi zao ambao walipata Pikipiki, Runinga na Katoni 50 za maji kwa watu 15 kwa kila zawadi hizo" ameeleza.
Aidha msimamizi huyo ameendelea kusema "Kwa wateja wa Maji ya Kilimanjaro nawaomba waendelee kutuunga mkono, wauze bidhaa zetu za maji ya kilimanjaro na siku kampuni ikisema tunarudisha kitu fulani kwa wateja wetu, basi wao watapewa kipaumbele".