Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Madaktari 44 waambukizwa Corona Hospitalini

Tuesday , 14th Jul , 2020

Madaktari 44 katika Hospitali ya kujifungulia kina mama, iliyopo Pumwani jijini Nairobi, wamekutwa na Corona na kupelekea mgomo baridi wa wahudumu wa afya, huku Serikali ikisema imeweka mikakati kuwakinga wahudumu hao.

Mkurugenzi Mkuu kutoka Wizara ya Afya Kenya, Dkt Patrik Amoth,

Madaktari hao wamebainika hii ni baada ya wafanyakazi 290 kupimwa hospitalini hapo, na kufikisha idadi ya wahudumu wa afya 429 ambao wamekwishaambukizwa Virusi vya Corona, ikiwa ni sawa na asilimia 4.1 ya maambukizi yote nchini Kenya.

Mkurugenzi Mkuu kutoka Wizara ya Afya Kenya, Dkt Patrik Amoth, alipotembelea Hospitali hiyo hii leo Julai 14, 2020, baada ya kuripotiwa kuwepo mgomo baridi hospitalini hapo, amethibitisha idadi hiyo ya maambukizi, na kusema kuwa wote waliokutwa na Corona wanaendelea vizuri.

"Kati ya watu 290 waliopimwa, 44 wamepatikana na Corona, bado tuna watu 100 ambao hatujawapima, lakini napenda niseme kuwa wote hao 44 wanaendelea vizuri, wako katika hali nzuri , na wengi hawajaonyesha dalili hivyo wanajitenga nyumbani kwao" amesema Dkt Amoth.

Licha ya hayo Serikali ya Kenya imesema kuwa haitaifunga Hospitali hiyo, kwa kuwa inategemewa na kina mama wengi nchini humo hasa wa Kaunti ya Nairobi, na kusisitiza tahadhari kuchukuliwa, ikiwemo ujenzi wa chumba maalum cha madaktari kutengwa na kupimwa ambao umekamilika.
 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton