
Pierre Aubameyang akishangilia goli alilofunga dhidi ya Manchester United
Aubameyang kwa sasa ndiye mchezaji anayelipwa zaidi ndani ya kikosi cha Arsenal, akitajwa kupokea zaidi ya fedha za Kitanzania bilioni moja kwa juma, na kuwa miongoni mwa wachezaji wa Kiafrika wanaolipwa vizuri Ulaya.
AFCON imekuwa na msisimko mkubwa tangu kuanza kwake 1957, kwa kuwa inakutanisha wachezaji bora wa Kiafrika wanaocheza ndani ya bara na nje ya bara, na limekuwa jukwaa pekee la kuoneshana umwamba kwa mataifa ya Afrika.
Gabon ipo kundi D lenye timu za Gambia, DR Congo pamoja na Angola, ikiwa na alama 4 sawa kabisa na Gambia yenye alama 4 pia, huku wakitofautiana wastani wa magoli, kwa maana hiyo hii mechi ina umuhimu mkubwa sana ndani ya kundi hilo.