Wednesday , 20th Jan , 2021

Baada ya kuachia ngoma yao mpya inayoitwa BABA ambayo ni collabo ya Stamina na Profesa Jay wakimshirikisha One Six, sasa Profesa ameeleza darasa walilotoa kwenye kiwanda cha muziki bongo.

Prof Jay na Stamina

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Profesa amesema sio lazima kuimba matusi na mambo ya kitandani na kuna nafasi kubwa ya kukiokoa kizazi.

BABA ni ngoma ambayo inafanya vizuri sana kwa hivi sasa ambapo kupitia mtandao wa YouTube ndio video inayotazamwa zaidi tangu ilipotoka ikiwa inashika namba moja kwa kuwa na watazamani zaidi ya laki tisa.