Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mpango wa JKT mbele ya Simba SC

Monday , 1st Mar , 2021

Ligi Kuu soka Tanzania bara itaendelea leo kwa mchezo mmoja ukiwa ni mzunguko wa 22 katika uwanja wa Benjamini Mkapa, mabingwa watetezi Simba SC watakuwa wenyeji wa JKT Tanzania ya Dodoma mchezo utapigwa majira ya Saa 1:00 usiku.

Ligi Kuu leo Simba Vs JKT Tanznaia

Simba wanaingia kwenye mchezo wa usiku wa leo wakiwa wanawazidi JKT Tanzania kwa tofauti ya alama 18, mabingwa hao watetezi wa VPL wekundu wa msimbazi ambao hawajapoteza mchezo hata mmoja kwenye michezo 5 ya mwisho ya Ligi kuu wakiwa wameshinda michezo 4 na sare mchezo 1, wapo nafasi ya pili wakiwa na alama 42, kwenye michezo 18.

JKT wamekusanya alama 24 kwenye michezi 21 wakiwa wanamiliki nafasi ya 10 kwenye msimamo, wameshinda michezo 3 kwenye michezo 5 ya mwisho ya ligi wamefungwa mchezo mmoja na wametoka sare mchezo mmoja.

Mchezo wa mkondo wa kwanza timu hizi zilipokutana mchezo ambao ulichezwa jijini Dodoma katika Dimba la Jamhuri Simba iliibuka na ushindi wa mabao 4-0, mabao ya Simba yalifungwa na Meddie Kagere ambaye alifunga mara mbili, mabao mengine yalifungwa na Chris Mugalu na Luiz Miquissone.

Kwenye michezo 5 ya mwisho timu hizi kukutana Simba wamekuwa na rekodi bora mbela ya JKT Tanzania kwani wameshinda michezo 4 na wamefungwa mchezo mmoja tu.

 

 

HABARI ZAIDI

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko

Serikali yaipongeza Red Cross

Waziri wa TAMISEMI Mohamed Mchengerwa

Aonya wanaochangia watumishi kutopanda madaraja

Edgar Lungu, Rais wa Zamani Nchini Zambia Akitembea Kuzunguka Mji Mkuu wa Lusaka

Rais wa zamani Zambia Bw. Lungu hatarini kukamatwa

Mkuu wa Ulinzi Ukraine (Picha ya Website)

Zelensky amfukuza kazi mkuu wake wa ulinzi

Baadhi ya Wananchi wa Chindi na Ntinga wakiwa katika Harakati za Kuvuka Mto

Walazimika kulipa hadi 8000 kuvuka mto kwa mtumbwi

Mohamedi Mchengerwa, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Wanaozuia watumishi kupanda vyeo wakaliwa kooni

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita