Tuesday , 9th Mar , 2021

Baadhi ya wanawake wilayani Serengeti mkoani Mara, wamelalamikia uwepo wa mila kamdamizi ya kuozeshwa mwanaume aliyefariki dunia maarufu kama ndoa ya makaburi jambo ambalo linawanyima haki na uhuru wa kuchagua mwanaume hivyo kufanya wanawake kuendelea kukandamizwa.

Wanawake Perepetua Njiku (Kushoto) na Christina Samwel

Wakizungumza na East Africa Television kwa nyakati tofauti, wanawake hao wamesema kuwa unakuta mtu ameshafariki dunia siku nyingi lakini jamii inalazimisha kwamba yule aliyefariki dunia awe na familia na kukuza ukoo licha ya kwamba alikwishatangulia mbele za haki siku nyingi na kuiomba serikali iingilie kati.
 
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Serengeti Nurdin Babu, amesema kuwa wanawake wengi wilaya ya Serengreti wanafanyiwa ukatili wa kijinsia na wananyamaza kimya.

Ndoa za makaburi ni maarufu kwa baaadhi ya makabila yaliyopo mkoani Mara, ambapo mwanaume anapofikia umri wa kuoa akafariki basi familia humuozesha mke ambaye akizaa watoto wanaitwa kwa jina la merehemu na dio maana zinaitwa ndoa za makaburi.