
Mwili wa Hayti Dkt. John Magufuli, ukipigiwa saluti na wanajeshi
Kabla ya mazishi ambayo yatafanyika saa 10:00 jioni ambayo yataongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, baadhi ya watu watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho mara baada ya misa takatifu ya kuaga mwili wa Hayati Dkt. Magufuli inayofanyika katika uwanja wa Magufuli uliopo Rubambagwe Chato.
Ambapo baadaye Rais Samia ataongoza familia na viongozi kuelekea eneo la mazishi ambapo ibada ya mazishi itaongozwa na Askofu Severine Niwemugizi.
Hayati Dkt. John Magufuli, alifariki dunia Machi 17, 2021, jijini Dar es Salaam katika hospitali ya Mzena kutokana na maradhi ya moyo