
Mwili wa Blandina ukiwa Kanisani
Ndugu, jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzake wa ITV/Radio One pamoja na wafanyakazi wengine wa makampuni wa IPP walishiriki Ibada hiyo na kutoa heshima zao za mwisho.
Baada ya ibada mwili wa marehemu Blandina ulianza safari ya kuelekea nyumbani kwao mkoani Mara kwa ajili ya maziko.
Waombolezaji wakiwa kanisani
Wakati wa uhai wake Marehemu Blandina alikuwa akiandaa na kutangaza kipindi Jarida la Wanawake, kinachorushwa na ITV.
Waombolezaji kwenye ibada ya kuaga mwili wa Blandina
Machi 28, 2021, mwili wake ulikutwa umetupwa njia panda ya ITV maeneo ya Mwenge Dar es Salaam na Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni kuthibitisha kuwa amefariki dunia.
Jeshi la Polisi limeeleza kwamba linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo la kuuawa mtangazaji huyo wa ITV Blandina Sembu.