
Khalid Mponda, Kaka wa marehemu Mariam Juma
Akizungumza na EATV Khalid Mponda, ambaye ni kaka wa marehemu amesema sababu iliyopelekea watoto hao kwenda mtoni na mmoja kukutwa na umauti ni kutafuta mifagio waliyokuwa wameagizwa shuleni.
"Aprili 25 majira ya jioni mama yao aliwazuia wasiende kule mtoni lakini baadaye wakamtoroka, wakakutana na wenzao walikuwa kama 17 sasa wakati wanavuka wakateleza mmoja akataka kumsaidia mwenzake na wote wakawa wametumbukia kwenye mto", amesema Kaka wa marehemu.
Katika hatua nyingine kaka wa marehemu ameleeza namna walivojitahidi kumtafuta marehemu siku ya kwanza ila hakupatikana mpaka waliporudi jana Machi 26, 2021, majira ya saa 12:00 asubuhi ndiyo akapatikana.