Tuesday , 7th Dec , 2021

Rapa Motra The Future anasema ngoma yake ya Weupe hajawa-diss Kikosi Kazi ila amewashauri kimuziki kwa sababu HipHop ni shule ya bure.

Picha ya msanii Motra The Future

Motra The Future ameongeza kusema wimbo wake huo wa Weupe ni kama amewakumbusha Kikosi Kazi kuacha kuwachana wasanii wenzao bali watafute michongo ya kuwaingizia pesa.

Wimbo wake huo kwa sasa upo trending namba 6 kwenye mtandao wa Youtube ukiwa na views 22,781.