(Baadhi ya wachezaji wa Taifa Stars wakiwa mazoezini kabla ya mchezo)
Mchezo huohautohusisha wachezaji kutoka timu za Simba na Yanga kama ilivyozoeleka kutokana na timu hizo kuwa na ratiba ya kukutana kwenye mchezp wa Kariakoo Derby Disemba 11, 2021 kwenye dimba la Mpaka.
Kuelekea kwenye mchezo huo, Mkurugenzi wa Michezo kutoka Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Yussuph Singo amesema maandalizi yamekamilika hivyo watanzania wajitokeze kwa wingi kwani kiingilio ni 2,000 tu
Kwa upande mwingine, Sherehe hizo pia zitaadhimishwa na wanasoka wanawake, ambapo timu ya taifa ya wanawake vijana chini ya miaka 20 ‘Tanzanite’ pia itacheza chini ya timu ya Uganda ya vijana saa 10:30 Jioni leo.
Kila tarehe 9 Disemba kila, Watanzania uungana popote walipo ili kusheherekea siku hiyo ambayo kwa sasa inajivunia kufanya mapinduzi makubwa ya kimaendeleo ikiwemo ya michezo yote kiujumla.