Friday , 29th Apr , 2022

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amekutana na viongozi wa masoko jijini Dar es salaam, kwa lengo la kujadili mbinu za kuzuia na kupambana na majanga ya moto masokoni huku vyanzo vya ajali hizo vikihusisha uzembe wa watu.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla

Aidha RC Makalla amesisitiza maboresho ya miondombinu kufanyika katika masoko yote Jijini Dar es salaam huku akiwataka wananchi kuacha kulilaumu Jeshi la zimamoto kwa kwa kuonekana hawafanyi kazi ipasavyo.

Kwa upande wao Wenyeviti wa masoko ya Mkoa wa Dar es salaam, wametaka zifanyikie juhudi kuwahamasisha wafanyabiashara kutumia nishati mbadala kama gesi, na kuachana na matumizi ya mkaa na kuni huku TANESCO wakitakiwa kufanya ukaguzi wa mitambo yao mara kwa mara.

Katika kipindi cha mwaka 2021/ 2022 masoko ya Jijini Dar es salaam  yalioungua ni pamoja na  soko la Kariakoo, soko la Mbagala, soko la Mchikichini, soko Mwenge la Cocacola na soko maalum la walemavu ilala boma.