
Waziri wa Maji Jumaa Aweso, akiwa na wake zake
Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 12, 2022, Bungeni Dodoma, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2021, ambapo wake zake wote wawili wamehudhuria bungeni kumshuhudia.
"Leo wake zangu wote wawili wamekuja hapa kuni-support haya sio mapenzi haya ni mahaba mazito sana, mimi ninawapenda sana ukiniona nachakarika ni kwa sababu ya ukaribu wao na ushirikiano mkubwa wanaonipa, mimi Jumaa Aweso nitaendelea kuwapenda sana wake wangu," amesema Waziri Aweso