
Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora ACP. Richard Abwao amesema Fisi huyo ambaye alizuka kutoka mahala pasipo julikana aliwavamia wanafamilia hao waliokuwa wakiendelea na shughuli zao shambani na kuwararua vibaya maeneo mbali mbali ya miili yao hasa katika upande wa mikono yao .
Kamanda amesema wakazi wa eneo hilo wamefanikiwa kumuua Fisi huo, huku hali ya majeruhi ikitajwa kuendelea vizuri baada ya kukimbizwa Hospitali kwa ajili ya matibabu .