Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watu 14 wafa kwa ajali ya moto Thailand

Friday , 5th Aug , 2022

Watu zaidi ya 14 wameuawa na wengine 41 kujeruhiwa baada ya moto kuzuka katika ukumbi wa burudani Mkoa wa Chonburi uliopo kusini -Mashariki mwa Thailand.

Taarifa ya polisi imebainisha kuwa moto huo umezuka majira ya saa saba usiku wa kuamkia leo katika klabu ya B nightspot katika wilaya ya Sattahip.

Kanda za video zilizosambaa mitandaoni zinaonyesha watu wanaokimbia wakitoka ndani ya klabu huku  wakipiga mayowe, wengine nguo zao zikiwaka moto.

Ukumbi huko Chonburi, jimbo lililoko kilomita 150 kusini mwa Bangkok, lilikuwa jengo la ghorofa moja lenye ukubwa wa mita za mraba 4,800.

Wazima moto walipambana kwa zaidi ya saa mbili ili kudhibiti moto huo,  na baada ya kuuzima waliikuta miili ya watu waliopoteza maisha katika maeneo mbalimbali ya klabu hiyo.

Wengine walipatikana karibu na kibanda cha DJ. Kufikia sasa, wote waliofariki wanaaminika kuwa raia wa Thailand.

HABARI ZAIDI

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini