
Kamisaa wa sensa ya watu na makazi Anna Makinda
Makinda amesema katika siku hizo mwananchi ambaye hajahesabiwa atapatiwa namba ya simu ambayo atapiga na kutoa taarifa zake kuanzia kesho
Amewataka wananchi ambao hawajahesabiwa katika zoezi hilo kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa makarani wa sensa watakaokuwa wanazungumza nao kwa njia ya simu ili kutoa taarifa zao
Katika hatua nyingine Kamisaa huyo wa sensa ya watu na makazi ametangaza kuanza sensa ya majengo nchi nzima ambayo itaanza mara tu baada ya kukamilika kwa zoezi la sensa ya watu na makazi
Akizungumzia changamoto zilizojitikeza wakati wa zoezi hilo ikiwemo vishkwambi kuisha umeme na baadhi ya makarani na wajumbe wa mtaa kutolipwa posho zao mkurugenzi wa huduma za sensa amesema hakuna mtu ambaye hatalipwa