Monday , 3rd Oct , 2022

Katika hali isiyo ya kawaida, Oktoba 2, nyuki walivamia ukumbi wakati uchaguzi ukiendelea wa kumpata Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Nyuki

Tukio hilo ambalo lilishangaza wengi, lilitokea wakati wa mapumziko wajumbe wakisubiri utaratibu wa kurudia uchaguzi baada ya wagombea kutofikia idadi ya kura stahiki. 

Kabla ya kurudiwa uchaguzi, wagombea walikuwa watatu akiwa ni Akimu Mwalupindi, Japhet Mwanasenga na Ramadhan Mwandala ambapo mshindi alipaswa kufikisha nusu ya kura ya wajumbe.

Katika kura za awali kabla ya uchaguzi kurudiwa, Mwalupindi alipata 682, Mwanasenga 500 na Mwandala akipata 218 na msimamizi kuamuru ngoma kurudiwa.

Wakati uchaguzi ukirudiwa hali ilibadilika ukumbini kwa kuzingirwa na nyuki wengi ambao haikufahamika walipotoka na kuwafanya wajumbe wengi kutawanyika na kukimbia bila kupiga kura.