Friday , 21st Oct , 2022

Takribani fimbo nyeupe Miatano zimekadhiwa kwa viongozi wa watu wasiyoona ikiwa ni jitihada za kuunga mkono serikali kutatua changamoto zinazowakabili walemavu wasioona haswa wale ambao hawana uwezo wakununua fimbo hizo

Naibu waziri wa Ajira Vijana Kazi na Watu Wenye Ulemavu Patrobas Katambi

Fimbo hizo zimekabidhiwa October 21 -2021 kwenye maadhimisho ya watu wasioona Duniani, ambapo kitaifa imefanyika katika mkoa wa Manyara wilayani Babati.

Katika maadhimissho hayo mgeni rasmi alikuwa Waziri mkuu Mhe.Kassim Majaliwa na akawakilishwa na Naibu waziri wa Ajira Vijana Kazi na Watu Wenye Ulemavu Patrobas Katambi ikiwa kauli mbiu ikisema “wasioona Tujumuishwe Katika Ajira michezo Teknolojia ya Habari na mawasiliano kwa maendeleo Endelevu“